Showing posts with label KURASA. Show all posts
Showing posts with label KURASA. Show all posts

Wednesday, May 8, 2019

Askofu Josephat Gwajima adai mkanda wa picha za ngono umetangenezwa na maadui zake

Askofu Josephat Gwajima


Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima nchini Tanzania, Josephat Gwajima amekanusha kuhusika na video ya ngono inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Kwa mujib wa Gwajima, video hiyo imetengenezwa na aliowaita maadui zake ambao wanalenga 'kumnyamazisha'.
Akiongea na wanahabari kwenye viunga vya kanisa lake jijini Dar es Salaam, Gwajima amesema msimamo wake na maono juu ya nchi ndiyo yamefanya kusingiziwa kashfa hiyo.
"Watu wanafanya haya ili nikose sauti. Wanasema 'tumpige Gwajima ili anyamaze.'" amesema na kuongeza: "Hizi picha zinajaribu kunichafua, lakini hawawezi."
Gwajima, ambaye pia amekuwa pia kwa namna moja ama nyengine akihusishwa ama kuhusika na siasa amesema: "Uchaguzi unakuja mwaka kesho (2020) na wanajua nina nguvu, hawataki niwe na sauti yoyote.
Hata hivyo, Gwajima hakuwataja kwa majina hao aliowaita kuwa ni maadui zake.
Video hiyo inayodaiwa kuwa ni ya Gwajima inamuonesha akiwa faragha na mwanamke wakifanya tendo la ngono. Na mtu anayedhaniwa kuwa ni Gwajima ndiye alikuwa akiichukua video hiyo kwa kutumia kamera ya mbele ya kifaa ambacho hakionekani.
"Ni mwanaume gani ambaye mwenye akili zake timamu anayeweza kujirekodi wakati akifanya tendo la ndoa? Haingii akilini," amejitetea Gwajima na kuongeza, "Zile ni picha za kuunganisha. Wametumia picha yangu moja ya kifamilia nikiwa kifua wazi na kuunganisha na picha nyengine ili wanichafue."
"...mkono wa huyo mtu anayejichukua ile video ni mkubwa, ni mkono wa 'baunsa' sio huu mkono wangu mdogo."
Gwajima pia amewaambia wanahabari kuwa tayari amesharipoti tukio hilo kwa mamlaka husika na kusema anatumai mtu aliyechapisha picha hizo kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram atakamatwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Askofu huyo aliambatana na viongozi wenzake wa kanisa lake pamoja na mkewe ambaye ameeleza kuwa ana imani na mumewe.
"...mimi ni jasiri kama Simba. Ukweli naufahamu. Mume wangu ninamfahamu na ninamwamini. Mungu akiwa upande wetu hakuna wa kutushinda," amesema Bi Gwajima.
Polisi waanza uchunguzi
Wakati huohuo, Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai (DCI), wameanza uchunguzi juu ya video ya ngono 'inayomhusisha' Askofu Gwajima.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo, Jumatano, Mei 8, 2019 na Kamanda wa polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, imeeleza kuwa Mei 7,2019 kuna video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na watu wasiojulikana ikionyesha mtu anayefanana na mchungaji huyo akiwa na mwanamke asiyefahamika.
"Jeshi la Polisi Kanda Maalumu limeanza uchunguzi wa video hiyo mara moja na linapenda kuwapa taarifa wananchi (kuwa) Gwajima siyo mtuhumiwa, ni muathirika wa tukio hilo kwani tukio hilo linaweza kufanywa na mtu yeyote kwa nia ya kutaka kuharibu heshima yake kwa jamii na waumini," amesema Mambosasa.
Taarifa hiyo imesema Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi kuacha kusambaza video hiyo kwa maelezo kuwa ni kosa la jinai na kuwataka waumini wa kanisa hilo kuwa watulivu kwani uchunguzi unaendelea ili kubaini aliyeisambaza na lengo la kufanya hivyo

Tuesday, May 7, 2019

Mfahamu kiongozi wa upinzani Afrika Kusini anayeandamwa na kivuli cha Mandela

Mmusi Maimane ndiye kiongozi wa kambi ya upinzani nchini Afrika Kusini.
Yeye ndiye kinara katika wa upinzani katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo ambao wachambuzi wanauita ni harakati ngumu za kutaka kumng'oa rais Cyrill Ramaphosa madarakani.


    Japo utawala wa kibaguzi ulikomeshwa rasmi Afrika ya Kusini mwaka 1994, mfumo wa vyama vya siasa kwa kiasi kikubwa, mifumo ya vyama vya siasa nchini humo imejengeka kulingana na Ni dhahiri kuwa, kuchaguliwa kwa Maimane kukiongoza DA imekuwa ni moja ya mbinu za chama hicho kuonekana ni cha wote na si kundi fulani ama rangi fulani.
    "Uweledi wa kiuongozi si jambo la uzoefu tu," ameiambia BBC na kuongeza, "Je, nimekuwa kisiasa toka nilipopata cheo hicho? Jawabu ni ndio."
    Na hivi karibuni aliwaambia wapinzani wake ndani na nje ya chama hicho 'wafunge midomo yao' kwa kumkosoa kuwa yeye ni kibaraka ama hana uzoefu wa kutosha.
    Presentational grey line
    Democratic Alliance leader Mmusi Maimane.Haki miliki ya pichaAFP
    Mambo saba kuhusu Mmusi Maimane
    • Alizaliwa mwaka 1980 kitongoji cha Soweto, Johannesburg ambapo Nelson Mandela aliishi kwa miaka mingi.
    • Amesoma vyuo vikuu nchini Afrika Kusini na Wales, ana Shahada ya Uzamivu katika masomo ya Teolojia na Saikolojia.
    • Ameoa mwanamke wa kizungu Natalie, ambaye walikutana kanisani, na kukiri kuwa ilimchukua muda kukubaliana na jamii inavyochukulia tofauti yao.
    • Anaongea lugha sita.
    • Amekuwa akihubiri kanisani jijini Johannesburg mwishoni mwa wiki kwa miaka kadhaa sasa.
    • Alikuwa mshauri wa kibiashara kabla ya kuingia kwenye siasa, na kuwa msemaji wa DA mwaka 2011.
    • Alichaguliwa kuwa kiongozi wa kwanza mweusi wa DA mwaka 2015 akiwa na miaka 34.
    Presentational grey line
    'Mapambano ya kihistoria'
    "Usipoteze kura yako tena kwa mtu mweupe," katibu mkuu wa ANC hivi karibuni amewaambia wapiga kura kwenye kampeni, akikilenga chama cha DA.
    Maafisa wa ANC, na wale wa chama kidogo lakini chenye msimamo mkali cha Economic Freedom Fighters (EFF), kinachoongozwa na Julius Malema, wanakishambulia wazi wazi chama cha DA kuwa si upinzani bali watumishi wa "mabepari weupe," na Bw Maimane kuwa ni "mfanyakazi wa bustani" anayelinda maslahi ya wazungu wachache.
    Mwaka 2005, Maimane alifunga ndoa na mwanamke wa Kizungu ambaye alikutana naye kanisani miaka kadhaa nyuma. Wana watoto wawili, wakike na wakiume.
    Kwa sasa Maimane anasema harakati dhidi ya ubaguzi nchini humo ni "mapambano yake ya kihistoria."
    "Bizo ndizo harakati zinazotawala Maisha yangu na nitazipambania mpaka siku nakufa," ameiambia BBC.
    Democratic Alliance members await the arrival of Mmusi Maimane on the campaign trail in Durban on 17 March 2019.Haki miliki ya pichaAFP
    Image captionCham cha DA kinataka kujivua dhana kuwa ni cha watu weupe waliowachache nchini Afrika Kusini
    Lakini mapambano hayo ya Maimane si kwa vyama pinzani tu, bali hata ndani ya DA.
    "Chama cha DA kililazimika kubadilika. Inabidi tuendelee kukibadilisha chama," amesema Maimane.
    Je anafanikiwa katika hilo?
    Wakosoaji wake wanasema uthabiti wa chama hicho umejengeka katika misingi yake ya kupambana kisera na utawala bora. Na kwakuwa Maimane aliingia uongozini akiwa hana uzoefu wowote, hivyo hana mchango mkubwa katika kukiimbarisha chama.
    Lakini kwa Maimane na wafuasi wake, wanasisitiza kuwa chini ya uongozi wake, chama hicho kimetanuka na kupenya katika maeneo na "jamii ambazo isingeweza kuzifikia hapo kabla."
    Kujikita katika siasa za uchumi
    Siku chache zijazo zitaamua mustakabali wa Maimane kisiasa.
    Mapambano makali zaidi yapo kwenye jimbo Tajiri zaidi nchini humo la Gauteng.
    Mmusi Maimane pictured with his wife, Natalie, in Cape Town ahead of the State of the Nation address on 16 February 2018.Haki miliki ya pichaAFP
    Image captionMmusi Maimane na mke wake, Natalie
    Chama cha DA ambacho tayari kinalishikilia jimbo la Western Cape, endapo kitaweza kuwashusha ANC mapaka chini ya 50% jimboni Gauteng, basi wataweza kuingia kwenye serikali ya mpito ya jimbo hilo.
    Ingawa kwa mwaka huu kura zote za maoni zinaonesha kuwa ANC watashinda uchaguzi, mchuoano wa Gauteng unatazamiwa kuamua uchaguzi wa kitaifa wa mwaka 2024.
    Katika miaka ya mwisho ya utawala wa rais aliyejiuzulu Jacob Zuma, chama cha ANC kilipoteza Imani miongoni mwa raia wengi wa nchi hiyo kutokana na kushamiri kwa kashfa za rushwa na ufisadi.
    Japo kwa sasa chama hicho kimeanza kurejesha Imani polepole chini ya rais Ramaphosa.

    Hata hivyo, Muimane anaamini ANC haiwezi kubadilika na imevunjika vipande vipande ambavyo haviwezi kuungika tena na kuwa kitu kimoja.
    Lakini pia nafahamu fika kuwa ni mapambano makli zaidi kuwaaminisha waliowengi nchini Afrika Kusini kuwa yeye na chama chake cha DA ndiyo mbadala na jibu kwa matatizo ya nchi.
    "Ninawaasa na kuwaomba Waafrika Kusini kuwezesha siasa za mrengo wa kati (chama cha DA) kushinda. Mabadiliko huwa hayapendezi sana mwanzoni, lakini tunayahitaji," amesema Maimane.
     za raia wake.